Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 90 | 2025-04-16 |
Name
Mwantatu Mbarak Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
House of Representatives
Primary Question
MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: -
Je, Serikali imewezaje kutatua changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP I)?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante sana, changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Kwanza (ASDP I) ni pamoja na miundombinu duni ya kilimo kwa maana ya barabara, maghala na miundombinu ya umwagiliaji; upatikanaji mdogo wa pembejeo kama mbegu bora, mbolea na viuatilifu; huduma duni za ugani; ushirikishwaji mdogo wa sekta binafsi; na upungufu wa takwimu sahihi za kilimo.
Mheshimiwa Spika, kutokana na hali hiyo, Serikali imezingatia katika kutatua changamoto hizo kupitia mipango inayoendelea kutekelezwa ukiwemo Mpango wa Muda Mrefu wa Mageuzi ya Sekta ya Kilimo kwa maana ya Tanzania Agricultural Master Plan - 2050. Maeneo ya kipaumbele yanayoendelea kutekelezwa kwa sasa ni kuendelea kuwekeza kwa kuimarisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo, huduma za ugani, utafiti, uzalishaji wa mbegu, kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao, upatikanaji wa masoko, kuimarisha upatikanaji wa takwimu na kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi ambao ulikuwa wa chini wakati wa utekelezaji wa ASDP I.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved