Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Finance and Planning | Wizara ya Fedha | 92 | 2025-04-16 |
Name
Katani Ahmadi Katani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tandahimba
Primary Question
MHE. CECILIA D. PARESSO K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -
Je, lini Serikali itarejesha fedha za miradi iliyochukuliwa na Hazina ili miradi hiyo iweze kukamilishwa?
Name
Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iramba Magharibi
Answer
WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 29 cha Sheria ya Bajeti, Sura 439, fedha ambazo hazijatumika hadi mwisho wa mwaka zinakoma matumizi yake mwisho wa mwaka unapofika. Lengo kuu la kanuni hiyo ni kusimamia uwajibikaji na uwazi katika matumizi ya fedha zilizotengwa katika bajeti.
Mheshimiwa Spika, hivyo, iwapo kuna miradi ama shughuli ambayo haijakamilika, Fungu husika linatakiwa kutenga bajeti na kuwasilisha maombi kwa kuambatisha hati za madai au nyaraka za utekelezaji wa miradi hiyo.
Mheshimiwa Spika, azma ya Serikali ni kuhakikisha kuwa miradi yote inatekelezwa ili kuleta maendeleo kwa wananchi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved