Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 94 | 2025-04-16 |
Name
Nancy Hassan Nyalusi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SYLVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la udumavu nchini?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na tatizo la udumavu nchini Serikali inatekeleza mpango kazi jumuishi wa masuala ya lishe wa mwaka 2021/2022 – 2025/2026 ambapo baadhi ya afua zinazotekelezwa ni kama ifuatavyo:-
(i) Uhamasishaji na umuhimu wa ulishaji sahihi wa watoto ikiwemo unyonyeshaji.
(ii) Utoaji wa elimu ya lishe katika vituo vya afya na uhamasishaji wa jamii kupitia vyombo vya habari.
(iii) Kwa wajawazito na wazazi/walezi wanapohudhuria kliniki.
(iv) Utoaji wa matone ya Vitamini A na dawa za minyoo kwa watoto wa umri wa chini ya miaka mitano.
(v) Uongezwaji wa virutubishi (madini na vitamini) katika vyakula hasa mafuta ya kula, unga wa ngano, unga wa mahindi na chumvi.
(vi) Utoaji wa vidonge vya madini chuma na asidi ya foliki kwa wanawake wajawazito.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved