Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 7 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 95 | 2025-04-16 |
Name
Lucy John Sabu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kuongeza vituo vya ushauri na programu za uhamasishaji ili kusaidia vijana na tatizo la afya ya akili?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali katika kupambana na tatizo la afya ya akili kama ifuatavyo: -
(i) Serikali inatoa huduma ya ushauri nasaha wa afya ya akili na uhamasishaji katika vituo vya afya 701 na hospitali zote za rufaa za mikoa pamoja na Hospitali ya Afya ya Akili Mirembe.
(ii) Serikali imefanya mafunzo kwa wataalamu 2,840 wakiwemo madaktari na wauguzi ili kuwawezesha kutambua na kushughulikia changamoto za magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo afya ya akili.
(iii) Serikali imeanzisha huduma ya call centre 115 ambapo pamoja na huduma nyingine, jamii inapata huduma ya ushauri nasaha ya afya ya akili kwa njia ya simu, lengo likiwa ni kuwafikia vijana wengi zaidi, kuwasaidia kwa haraka na pia kupunguza unyanyapaa kwa wale wasiopenda kwenda hospitalini moja kwa moja.
(iv) Serikali imeanzisha vituo 1561 vya kutoa huduma rafiki kwa vijana katika mikoa yote, ikiwemo huduma za afya ya akili kupitia Mkakati Jumuishi wa Vijana (NAIA).
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved