Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Lucy John Sabu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY J. SABU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuongeza vituo vya ushauri na programu za uhamasishaji ili kusaidia vijana na tatizo la afya ya akili?
Supplementary Question 1
MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja dogo la nyongeza. Kumekuwepo na changamoto kubwa kwa vijana ambao wamekosa ajira, hivyo kusababisha kuwa na msongo wa mawazo na afya ya akili. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia tatizo la afya ya akili kabla kijana hajakumbwa na changamoto hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, vilevile Serikali inatumia gharama kubwa katika kuwahudumia vijana hawa. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba changamoto hii inakwisha kabisa? (Makofi)
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, matatizo ya akili yanayosababishwa na ukosefu wa ajira, ninafikiri tunaweza tukayakabili. Moja, kwa kuelemishana namna sahihi ya kufikiri na kuyatazama maisha. Ndiyo maana Serikali imekuja na mtaala mpya wa kuyarekebisha masuala ya elimu, ili mtu toka akiwa mtoto, chekechea, basi ajitambue na ajue kwamba, unaposoma hata usipoajiriwa kuna namna nyingine ya kufanya ukaweza kuzalisha na ukaishi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved