Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 262 | 2025-05-09 |
Name
Atupele Fredy Mwakibete
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busokelo
Primary Question
MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza: -
Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya Mpata, Isange na Ntaba – Busokelo?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Mpata, Isange na Ntaba jumla ya shilingi milioni 491 zinahitajika. Kituo cha Afya Mpata kinahitaji shilingi milioni 395, Kituo cha Afya Isange shilingi milioni 76 na Kituo cha Afya Ntaba shilingi milioni 20.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imetoa shilingi milioni 150 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Vituo vya Afya vya Mpata, Isange na Ntaba katika Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi viporo ya vituo vya afya nchini ikiwa ni pamoja na Vituo vya Afya vya Mpata, Isange na Ntaba, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved