Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 263 | 2025-05-09 |
Name
Ndaisaba George Ruhoro
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngara
Primary Question
MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza kuwawezesha Maafisa Ugani kwa kuwapa mafuta ili waweze kutembelea wakulima?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua majukumu muhimu yanayofanywa na Maafisa Ugani katika kutekeleza majukumu yao kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa. Ili kuwawezesha Maafisa Ugani kutekeleza majukumu yao katika halmashauri, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo mpaka kufikia Machi, 2025 imewapatia wataalamu hao vitendea kazi mbalimbali zikiwemo pikipiki 6,444, vishikwambi 5,426, sare 6,456 na magari 40.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2025/2026 jumla ya mikoa mitano, halmashauri 12 zimetenga bajeti ya mafuta kati ya lita 10 hadi 15 kwa kila mwezi kwa ajili ya kuwawezesha Maafisa Ugani kutekeleza majukumu yao. Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri zitaendelea kutenga bajeti ya fedha kwa ajili ya mafuta na matengenezo ya pikipiki za Maafisa Ugani ili waweze kutekeleza majukumu yao na kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri husika, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved