Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 264 | 2025-05-09 |
Name
Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Ilemela
Primary Question
MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga uzio katika Shule za msingi ambazo hazina uzio maeneo ya mijini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kujenga uzio katika shule mbalimbali za msingi kwa kuzipa kipaumbele shule zenye watoto wenye mahitaji maalumu. Katika mwaka 2022/2023 na 2023/2024 Serikali imetoa shilingi bilioni 5.57 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika shule 185 za watoto wenye mahitaji maalumu. Vilevile, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikitenga fedha kupitia mapato ya ndani kujenga uzio ili kuimarisha ulinzi katika maeneo yenye changamoto za kiusalama. Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri itaendelea kutenga fedha za ujenzi wa uzio kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na mali za shule kadiri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved