Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 266 | 2025-05-09 |
Name
Bupe Nelson Mwakang'ata
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA Aliuliza: -
Je, lini Mradi wa Umwagiliaji Bonde la Rukwa wenye thamani ya shilingi bilioni 21 utakamilika?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ujenzi wa Skimu ya Ilemba wenye thamani ya shilingi bilioni 21 ulitarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2024. Hata hivyo, ujenzi huo haukukamilika kutokana na mvua za El-Nino za mwaka 2023/2024 pamoja na mvua nyingi za masika zinazoendelea mkoani Rukwa kwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imefanya tathmini ya muda uliopotea kutokana na mvua nyingi zilizosababisha kusimama kwa kazi na kuongeza muda wa utekelezaji wa mradi hadi mwezi Disemba, 2025. Ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa muda uliopangwa, Tume itaendelea kumsimamia mkandarasi husika kwa karibu. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved