Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 267 | 2025-05-09 |
Name
Salim Mussa Omar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Gando
Primary Question
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI K.n.y. MHE. SALIM MUSSA OMAR Aliuliza: -
Je, ni upi mpango wa Serikali kuifanya NFRA kujitegemea hususan Idara ya Vyakula ili kuepuka uhaba wa chakula pindi nchi tegemezi zinapokumbwa na majanga?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO Alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuimarisha uwezo wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) ili ijitegemee na kupunguza utegemezi wa Serikali bila kuathiri jukumu lake la msingi la kuhakikisha usalama wa chakula nchini, Serikali ina mikakati ifuatayo:-
(i) Kuongeza uwezo wa kuhifadhi chakula kutoka tani 776,000 wa sasa hadi tani 3,000,000 ifikapo mwaka 2030. Hatua hiyo itafikiwa kwa kukarabati na kujenga vihenge na maghala ya kisasa na hivyo kuwezesha kudhibiti upotevu wa mazao baada ya mavuno;
(ii) Kuimarisha mifumo ya ununuzi na usambazaji ikiwemo matumizi ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi na kuhakikisha upatikanaji wa chakula kwa haraka katika maeneo yenye changamoto; na
(iii) Kuimarisha uwezo wa kibajeti kwa kuongeza vyanzo vya mapato ikiwemo uzinduzi wa Hati Fungani ya Usalama wa Chakula (Food Security Bond). Hati hii inalenga kuongeza mtaji kwa ajili ya uboreshaji zaidi wa miundombinu, upanuzi wa shughuli za kibiashara na utekelezaji wa mikakati ya muda mrefu ya usalama wa chakula nchini.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved