Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 270 | 2025-05-09 |
Name
Justin Lazaro Nyamoga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. JUSTIN L. NYAMOGA Aliuliza: -
Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga Kiwanda cha Chai cha Kilolo?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, Serikali kwa kutambua umuhimu wa uwepo wa Kiwanda cha Chai Kilolo imefanikiwa kuvutia uwekezaji wa kiwanda hicho na uwekezaji umefanywa na Kampuni ya HongDingXin ya kutoka China. Kiwanda kina uwezo wa kuchakata tani 20 za chai kwa siku na kitatoa ajira 120 za moja kwa moja pamoja na kutoa soko la uhakika kwa wakulima wa chai katika Wilaya ya Kilolo na maeneo ya jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa ujenzi wa kiwanda hicho umekamilika na tayari wameshaanza majaribio tangu tarehe 28 Aprili, 2025, mara baada ya majaribio hayo kukamilika, tunaamini mpaka sasa watakuwa wameanza uzalishaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved