Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 273 | 2025-05-09 |
Name
Boniphace Nyangindu Butondo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kishapu
Primary Question
MHE. BONIPHACE N. BUTONDO Aliuliza: -
Je, lini usambazaji wa maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Mondo, Busangwa, Sekebugolo na Mwasubi - Kishapu utakamilika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, Serikali imekamilisha usanifu wa kina wa mradi wa kutumia maji ya Ziwa Victoria kwenda kwenye Kata za Wilaya ya Kishapu ikiwemo Kata za Mondo, Busangwa, Sekebugolo na Mwasubi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la mradi huo ni kutatua changamoto ya huduma ya maji katika kata hizo ambapo kiasi cha shilingi bilioni 16.1 kinahitajika. Kwa sasa Serikali inaendelea na utafutaji wa fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo. Aidha, kwa sasa huduma ya maji inapatikana kwa baadhi ya maeneo ya kata hizo kupitia visima vya pampu za mkono 12, Bwawa la Sekeididi pamoja na mtandao wa mabomba wa zamani.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved