Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 10 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 123 | 2025-04-23 |
Name
Dr. Thea Medard Ntara
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-
Je, SIDO ina mpango gani kukopesha Wajasiriamali vifungashio kama ambavyo benki zinavyokopesha fedha ili kuongeza ubora wa bidhaa?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ajliibu:-
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Serikali kupitia SIDO huwarahisishia Wajasiriamali kupata vifungashio kwa kununua kwa jumla (bulk procurement) na Wajasiriamali kuweza kupata vifungashio hivyo katika ofisi za SIDO mikoani kwa kuuziwa rejareja na kwa bei nafuu. Utaratibu huo umewawezesha Wajasiriamali kupata vifungashio kwa wakati na kwa kutumia mikopo ya NEDF inayotolewa na SIDO.
Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa upatikanaji wa vifungashio kwa wajasiriamali, Serikali imeendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya vifungashio hapa nchini ili kurahisisha upatikanaji wake na kwa bei nafuu. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved