Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:- Je, SIDO ina mpango gani kukopesha Wajasiriamali vifungashio kama ambavyo benki zinavyokopesha fedha ili kuongeza ubora wa bidhaa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, kwa sasa hivi vijana wengi sana hasa waliomaliza vyuo wamejishikiza katika ajira ya ujasiriamali na wanahitaji vifungashio. Swali la kwanza; je, SIDO imefanya tathmini ya changamoto zinazowakabili wajasiriamali wadogo na hasa hao vijana waliotoka vyuo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, SIDO haioni haja ya kuwa na utaratibu wa kushirikiana na taasisi za kifedha ili wanufaika wa mafunzo hasa vijana waweze kupata mitaji ya kuanzisha au kupanua shughuli zao za kiuchumi? Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana na kumshukuru Mheshimiwa Ntara kwa weledi na ushauri wake na huyu ni daktari msomi maana yake amesema kwamba vijana wajasiriamali wengi wana changamoto ya mtaji.

Mheshimiwa Spika, SIDO moja ya kazi zake ni kufanya au kuendeleza teknolojia mbalimbali za viwanda, lakini pia wanatoa mafunzo na uendelezaji wa biashara. Zaidi, wanafanya kutafuta masoko na uwekezaji na zaidi ni hii ambayo Mheshimiwa Mbunge amesema kuhusiana na mikopo ya kifedha kwa vijana na wajasiriamali wengine.

Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue ushauri wake kwamba SIDO sasa tuna nafasi ya ziada ya kufanya tathmini ya kina ili kuhakikisha tunaona changamoto zilizopo kwa vijana na hasa kwenye sehemu hii mahususi ya vifungashio. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili, tayari Serikali kupitia SIDO inashirikiana na baadhi ya taasisi za kifedha kupitia mifumo hasa hivi viwanda ambao unasaidia, lakini mahususi unakwenda kwenye viwanda vikubwa au vya kati ambavyo wajasiriamali wengi hawana uwezo huo wa kukopa zaidi ya shilingi milioni tano na kuendelea. Kwa hiyo nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwamba tunachukua ushauri wake, lakini zaidi tutaendelea kuboresha kwa kuhamasisha ujenzi wa viwanda zaidi hapa nchini vya vifungashio, ambalo ndiyo tatizo kubwa katika nchi yetu kwa bidhaa ambazo ni nzuri zinazozalishwa. Kwa sababu bidhaa inaweza kuwa nzuri lakini ukifungasha kwenye kifungashio ambacho hakivutii au hakina ubora maana yake hata thamani ya bidhaa hiyo inakuwa ni ndogo. Ninakushukuru. (Makofi)