Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 10 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 125 2025-04-23

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kusafisha na kuweka uzio Uwanja wa Ndege Urambo kwa kuwa ni muhimu kwa Biashara ya Tumbaku na ni Uwanja wa dharura?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inakubaliana na pendekezo la ujenzi wa uzio ili kuimarisha usalama katika Kiwanja cha Ndege Urambo na tayari suala hili limejumuishwa katika Rasimu ya Mpangomkakati wa TAA wa miaka mitano ijayo ili kutoa wigo wa matumizi ya rasimalifedha inayotengwa katika bajeti ya miradi ya maendeleo kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya ukarabati na upanuzi wa viwanja vya Ndege ikiwemo Ujenzi wa Jengo Jipya la Abiria katika Kiwanja cha ndege cha Tabora ambalo ujenzi wake umefikia 94.1%.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na uhakikishaji wa Kiwanja cha Ndege cha Urambo kipo salama, TAA inaendelea na utekelezaji wa maagizo ya kitaifa kuhusiana na ulinzi na usalama, ikiwemo na ushirikishwaji wa wananchi ili kulinda mipaka kupitia uhamasishaji wa ulinzi shirikishi. Hali kadhalika, kiwanja hiki kina hati miliki ili kuepuka uvamizi wa ardhi unaoweza kufanyika kutokana na idadi ndogo ya shughuli za kiuendeshaji zinazofanyika kiwanjani hapo.