Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 10 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 127 2025-04-23

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali wa kuimarisha kilimo cha alizeti katika Wilaya ya Kakonko?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kakonko ni miongoni mwa maeneo yanayofaa kwa kilimo cha zao la alizeti. Katika kuimarisha kilimo cha alizeti Wilayani Kakonko, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora, kuwapa vitendea kazi Maafisa Ugani ili waweze kuwafikia wakulima na kutoa ushauri wa kilimo bora cha alizeti.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza mikakati hiyo, katika msimu wa Mwaka wa Fedha 2024/2025, Halmashauri ya Kakonko imeanzisha mashamba manne ya mbegu katika Kata za Kiziguzigu na Rulenge. Pia, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetoa pikipiki 13 na kifaa cha kupima afya ya udongo (soil scanner) kwa Maafisa Ugani. Kifaa hicho kitawezesha kushauri wakulima matumizi sahihi ya mbolea.

Mheshimiwa Spika, baada ya kutekeleza mikakati hiyo na uzalishaji kuongezeka, Serikali itaendelea kuhamasisha wawekezaji kuanzisha viwanda vya kuzalisha mafuta ya kula. (Makofi)