Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 10 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 129 | 2025-04-23 |
Name
Ng'wasi Damas Kamani
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia Wahitimu waliosoma katika Vyuo vya Jumuiya ya Afrika Mashariki kupata usajili ili kuajiriwa nchini?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, usajili wa wahitimu kutoka vyuo vya nje ya nchi ikiwa ni pamoja na Vyuo vya Jumuiya ya Afrika Mashariki hufanywa na Mamlaka za Usajili au Bodi za Kitaaluma (Professional Bodies), kwa kuzingatia taratibu zilizopo. Kabla ya usajili mhitimu hutakiwa kupeleka vyeti vya taaluma Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na wale wa stashahada na cheti hupeleka vyeti Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET), ili kufanya uthibitisho, ulinganifu wa sifa na kiwango cha elimu. Hivyo ninapenda kuwasihi wahitimu wote kutoka vyuo vya nje ya nchi kufuata utaratibu uliopo, ili kupata usajili. Ninakushukuru sana. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved