Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 152 | 2025-04-28 |
Name
Flatei Gregory Massay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Vijijini
Primary Question
MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -
Je, lini Serikali itasikiliza malalamiko ya watumishi dhidi ya Kikokotoo?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuwa sikivu muda wote kunapojitokeza hoja zinazohusu kikokotoo cha mafao kwa wastaafu. Katika kuonesha usikivu wake, kuanzia Julai, 2024 Serikali imeongeza malipo ya mkupuo kutoka 33% hadi 40% kwa wastaafu na kuanzia mwezi Januari, 2025 Serikali imefanya mabadiliko katika malipo ya pensheni kwa wastaafu kwa kupandisha kiwango cha chini cha pensheni kutoka shilingi 100,000 hadi 150,000 kwa Mifuko yote miwili, PSSSF na NSSF.
Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kuonesha usikivu huo, Serikali imepandisha kiwango cha malipo ya pensheni kwa mwezi kwa wastani wa asilimia mbili kwa mwaka na kuwa Mifuko imeanza kulipa ongezeko hilo tangu mwezi Januari, 2025.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved