Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 154 2025-04-28

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU K.n.y. MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya vya kimkakati kwenye Kata za Isuna, Mang'onyi na Siuyu?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeandaa mpango wa ujenzi wa vituo vya afya katika Kata za kimkakati kwa awamu. Katika mwaka 2024/2025, Serikali imetenga shilingi milioni 250 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya kwenye Kata ya Misughaa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Isuna. Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya katika Kata za Kimkakati zikiwemo Kata za Mang'onyi na Siuyu.