Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 156 | 2025-04-28 |
Name
Michael Constantino Mwakamo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibaha Vijijini
Primary Question
MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kutenga Shule chache za Kata kuwa za bweni kwa kuwa, matokeo ya wanafunzi si mazuri?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa shule kuwa na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia, ikiwemo uwepo wa mabweni. Katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2023/2024 – 2024/2025, Serikali imetumia shilingi bilioni 70.33 kujenga mabweni 537 katika shule za kata 270, ili zipandishwe hadhi kuwa kidato cha tano na sita. Kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni ujenzi wa shule mpya za kutwa ili kupunguza msongamano wa wanafunzi na watoto kutembea mwendo mrefu na kuongeza nafasi katika shule za kidato cha tano na sita.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved