Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 13 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 159 2025-04-28

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ukarabati wa Mahakama za Mwanzo West Meru na Nkoaranga, ambazo zimeachwa na kubakia magofu?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania imeendelea kutekeleza mpango wake wa ujenzi na ukarabati wa Majengo ya Mahakama wa mwaka wa fedha 2021/2022 – 2025/2026 kwa kuimarisha majengo katika ngazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenga majengo mapya na kukarabati yaliyopo. Majengo haya yanajengwa na kukarabatiwa kwa awamu kwa kuzingatia Mpango wa Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Mahakama na kadri ya fedha zinavyopatikana.

Mheshimiwa Spika, ukarabati wa Mahakama ya Mwanzo Nkoaranga na Mahakama ya Mwanzo West Meru utafanyika kwa bajeti ya 2025/2026. Aidha, kutokana na mahitaji makubwa katika jimbo la Arumeru, mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali imejenga jengo la kisasa la Mahakama ya Mwanzo Maji ya Chai, na lipo katika hatua za mwisho kukamilika.