Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ukarabati wa Mahakama za Mwanzo West Meru na Nkoaranga, ambazo zimeachwa na kubakia magofu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina swali moja la nyongeza. Kata za Ngalinanyuki, Uwiro, na Ngabobo ziko nyuma ya mlima Meru Kaskazini ambako ni mbali sana na mahakama ya mwanzo ya maji ya chai. Je, Serikali ina tamko gani kuhusu ukarabati wa Mahakama ya Mwanzo iliyoko Ngarenanyuki?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumefanya katika Mahakama ya Maji ya Chai pamoja na Oldonyosambu, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakwenda kuhakikisha kwamba tunafanya ukarabati katika Mahakama hii ya Ngarenayuki kwa fedha ambayo tutapitisha kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha 2025/2026.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ukarabati wa Mahakama za Mwanzo West Meru na Nkoaranga, ambazo zimeachwa na kubakia magofu?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, Kata ya kikunde na Kata ya Pabi halikadhalika na Kata ya Tuhuli zina umbali takribani kilomita 80 kutoka Makao Makuu ya Wilaya ambapo kuna Mahakama ya Mwanzo. Je, kuna mpango mkakati gani wa kuhakikisha kwamba kata hizi zinakuwa na Mahakama za Mwanzo?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimesema, Agosti 2022 Mahakama ilizindua mpango wa ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Mahakama. Mpango huo haujaacha kata yoyote, tarafa yoyote wilaya yoyote na mkoa wowote. Kata ya Kinguli na kata zingine kwa Mheshimiwa Omari nao umezingatiwa katika mpango na tutafanya ukarabati.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ukarabati wa Mahakama za Mwanzo West Meru na Nkoaranga, ambazo zimeachwa na kubakia magofu?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninataka kufahamu, je, wamefikia hatua ipi katika ujenzi wa Mahakama katika Wilaya ya Ileje?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Mahakama katika Wilaya ya Ileje unaendelea na tunategemea kwamba utakamilika mwaka ujao wa fedha.