Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 13 Finance Wizara ya Fedha 160 2025-04-28

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuanza ujenzi wa Kituo cha Forodha Kijiji Mukikoro Kata ya Mugoma – Ngara?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha ujao wa 2025/2026, Serikali ina mpango wa kujenga jumla ya vituo sita vya forodha mipakani na imekwishakutenga jumla ya shilingi bilioni 1.1. Kati ya vituo hivyo Kituo cha Forodha Mugoma - Ngara kitajengwa maeneo ya Mugoma, katika Wilaya ya Ngara, mpakani mwa Tanzania na nchi ya Burundi, ahsante.