Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuanza ujenzi wa Kituo cha Forodha Kijiji Mukikoro Kata ya Mugoma – Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninalo swali moja la nyongeza. Mchakato wa ujenzi wa kituo hiki cha forodha katika Kijiji cha Mkikomero Kata ya Mugoma, Wilaya ya Ngara ulianza una miaka zaidi ya miwili sasa tangu uanze. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa kituo hicho ili kuweka hata makontena tusiendelee kupoteza mapato katika Serikali yetu?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninaomba nimpongeze sana Mheshimiwa Oliver kwa kazi kubwa sana na juhudi anayofanya katika ufuatiliaji wa ujenzi wa kituo hicho. Ninaomba nimhakikishie kwamba juhudi yake imezaa matunda mazuri na hivi karibuni kwa sababu fedha imekwishatengwa kituo hicho kitaanza kujengwa mara tu baada ya mwaka wa fedha unaokuja.