Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 13 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 162 2025-04-28

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza:-

Je, nini mpango wa Serikali kuendeleza Bandari ya Kyamkwikwi na kujenga barabara ya kuunganisha Bandari na Barabara Kuu?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TPA imekamilisha kazi ya kuhuisha Mpango Kabambe wa Mwaka 2021 - 2045 wa Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari Nchini.

Mheshimiwa Spika, Mpango huo umeainisha mahitaji ya uendelezaji wa Bandari nchini ikiwa ni pamoja na Bandari ya Kyamkwikwi katika Ziwa Victoria. Mpango Kabambe huo unatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano mitano ambapo kwa sasa TPA imeanza na ujenzi wa Gati la kuhudumia shehena na abiria katika maeneo hayo.