Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 162 | 2025-04-28 |
Name
Charles John Mwijage
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba Kaskazini
Primary Question
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza:-
Je, nini mpango wa Serikali kuendeleza Bandari ya Kyamkwikwi na kujenga barabara ya kuunganisha Bandari na Barabara Kuu?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TPA imekamilisha kazi ya kuhuisha Mpango Kabambe wa Mwaka 2021 - 2045 wa Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari Nchini.
Mheshimiwa Spika, Mpango huo umeainisha mahitaji ya uendelezaji wa Bandari nchini ikiwa ni pamoja na Bandari ya Kyamkwikwi katika Ziwa Victoria. Mpango Kabambe huo unatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano mitano ambapo kwa sasa TPA imeanza na ujenzi wa Gati la kuhudumia shehena na abiria katika maeneo hayo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved