Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 164 | 2025-04-28 |
Name
Hawa Mchafu Chakoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-
Je, nini kauli ya Serikali juu ya changamoto ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Kipugila Rufiji?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Kata ya Kipugila, inapata huduma ya mawasiliano kupitia minara iliyojengwa katika Vijiji vya Kipo kwa mnara wa Halotel na Kipugila mnara wa TTCL.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu jitihada za Serikali katika kutatua changamoto ya mawasiliano katika kata hii, inaashiria kuwa bado kuna changamoto. Wizara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itafanya tathmini kwenye kata hii ili kubaini mahitaji halisi ya mawasiliano na endapo ikibainika kuwepo kwa tatizo la mawasiliano katika kata husika, itaingizwa katika zabuni ya miradi itakayotekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2025/2026.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved