Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Community Development, Gender and Children | Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum | 165 | 2025-04-28 |
Name
Fakharia Shomar Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI K.n.y. MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Je, nini kauli ya Serikali juu ya Wanawake wanaotupa watoto?
Name
Mwanaidi Ali Khamis
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inakemea na kulaani kitendo cha baadhi ya wanawake kutupa watoto kwa lengo la kukwepa jukumu lao la msingi la kusimamia malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto. Hivyo, ninapenda jamii itambue kuwa Serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya wanawake watakaokutwa na hatia ya kutenda kosa hilo na kuadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto, Sura ya 13, Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 pamoja na sheria nyingine za nchi zilizotungwa kwa suala hilo.
Mheshimiwa Spika, ninawasihi wanawake na jamii kwa ujumla kuacha tabia ya kutupa watoto. Aidha, endapo itatokea kuna mtu ameshindwa kutekeleza jukumu la malezi ya mtoto basi atoe taarifa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hususani Ofisi za Ustawi wa Jamii ambapo watawajibika kuweka mpango wa huduma mbadala kwa mtoto husika sawa na matakwa ya kifungu Na. 94(5) cha Sheria ya Mtoto Sura ya 13. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved