Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 13 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 166 | 2025-04-28 |
Name
Fatma Hassan Toufiq
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FATMA HASSAN TOUFIQ aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha upimaji wa ardhi unafanyika katika Vijiji vyote Tanzania Bara?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, katika ardhi za vijiji, jumla ya vijiji 10,987 kati ya vijiji 12,333 vilivyosajiliwa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI vimepimwa mipaka yake. Vijiji vilivyoandaliwa Mipango ya matumizi bora ya ardhi ni 4,346 sawa na 35.24% ya vijiji 12,333. Uandaaji wa mipango hiyo umewezesha kutambua vipande vya ardhi 259,080 na kutolewa hatimiliki za kimila.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha kupitia bajeti ya Serikali ambapo kila mwaka Serikali hutenga fedha kwa ajili ya kazi hiyo. Ni matarajio ya Serikali kukamilisha zoezi hili kutegemea upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved