Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 167 | 2025-04-29 |
Name
Tauhida Cassian Gallos Nyimbo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Wazee kuanzia umri wa miaka 60 nchini wanaingia katika Mfumo wa Hifadhi ya Jamii?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60 wanaendelea kunufaika na Mfumo wa Hifadhi ya Jamii hapa nchini, Serikali imeweka utaratibu wa kuwawezesha wazee waliokuwa katika Sekta Binafsi kuendeleza uanachama wao katika Mfuko wa NSSF hadi kufikia miaka 70. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved