Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 168 | 2025-04-29 |
Name
Priscus Jacob Tarimo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Moshi Mjini
Primary Question
MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha Mradi wa Stendi ya Ngangamfumuni - Moshi Mjini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Ujenzi wa Stendi ya Ngangamfumuni katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ulianza kutekelezwa mwaka 2019 kwa Mkataba wa shilingi bilioni 28.9 ambapo hadi sasa jumla ya shilingi bilioni 7.5 zimetolewa na mradi umefikia 51% ya utekelezaji. Aidha, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetenga bajeti ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya uendelezaji wa ujenzi wa mradi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutoa fedha za ujenzi wa stendi hii, kadri hati za malipo zitakavyokuwa zikiwasilishwa hadi mradi utakapokamilika. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved