Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 169 | 2025-04-29 |
Name
Festo Richard Sanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Makete
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Stendi ya Kisasa – Makete kupitia miradi ya kimkakati ya Serikali?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kujenga na kuboresha stendi za mabasi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini kwa awamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Makete inayo stendi yenye eneo la ukubwa ekari 3.1 katika eneo la Mabehewani. Stendi hii iliboreshwa na Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri, ambapo kiasi cha shilingi milioni 40 kilitumika na stendi hii inatumia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri ya Makete imetenga shilingi milioni 100 ili kuboresha miundombinu ya Stendi ya Mabehewani. Aidha, ili kuwa na stendi kubwa ya kisasa zaidi, Halmashauri ya Makete imetenga eneo la ekari 24.5 na sehemu ya eneo hilo itatengwa kwa ajili ua ujenzi wa stendi ya kisasa. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved