Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 170 | 2025-04-29 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-
Je, lini Serikali itamaliza changamoto ya upungufu wa Walimu wa Masomo ya Hesabu na Physics shule ya Sekondari Bukene?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejenga shule mpya ya Sekondari Mbale ambayo imesaidia kupunguza idadi ya wanafunzi katika shule ya Bukene kutoka 589 (wavulana 262 na wasichana 327) hadi 488, (wavulana 203 na wasichana 285), hivyo kupunguza tatizo la ikama ya walimu katika shule hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Sekondari Bukene ina uhitaji wa Mwalimu mmoja wa Fizikia, waliopo ni watatu. Hisabati uhitaji ni mwalimu mmoja, waliopo ni watatu. Hivyo, shule hii haina upungufu wa walimu wa masomo ya fizikia na hisabati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuendana na ongezeko la shule na idadi ya wanafunzi, Serikali itaendelea kuajiri walimu kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved