Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 171 | 2025-04-29 |
Name
Tumaini Bryceson Magessa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Primary Question
MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaboresha miundombinu ya barabara katika Mji Mdogo wa Katoro ikiwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya tathmini na kubaini kuwa zinahitajika zaidi ya shilingi bilioni 15 ili kuboresha miundombinu ya Mji wa Katoro, ikiwemo ujenzi wa lami kilometa 10, changarawe kilometa 20 na mitaro kilometa 12.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza uboreshaji wa miundombinu ya Mji huo kwa kujenga mitaro kilometa nane na ukarabati wa barabara kilometa nane kwa kiwango cha changarawe kupitia Mradi wa Dharura (CERC), kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, wenye thamani ya shilingi bilioni 1.2.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa mchakato wa ununuzi upo kwenye hatua za mwisho za kumpata mkandarasi atakayetekeleza kazi hiyo. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved