Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 547 | 2025-06-10 |
Name
Dorothy George Kilave
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Temeke
Primary Question
MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuyatambua maeneo yote yanayoathiriwa na maafa na kuweka mkakati wa ziada?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Temeke kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza hatua mbalimbali za kimkakati katika kuyatambua maeneo yaliyoathirika na maafa pamoja na kuweka mikakati ya muda mfupi na mrefu kupunguza athari za maafa hayo kwa kuzingatia Sera ya Menejimenti ya Maafa ya mwaka 2004, Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022 pamoja na miongozo ya kitaifa na kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ambazo Serikali imezichukua ili kutambua maeneo yenye maafa na kupunguza madhara ya maafa hayo ni pamoja na kuandaa Wasifu wa Majanga wa mwaka 2019 ambao umeainisha maeneo yote yaliyo katika hatari; kufanya tathmini ya vihatarishi vya maafa katika Wilaya 36 na kuimairisha mifuko ya ufuatiliaji wa mwenendo wa majanga, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved