Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 172 | 2025-04-29 |
Name
Ritta Enespher Kabati
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:-
Je, Serikali inatambua biashara ya mtandao na Makampuni mangapi yamejisajili na mapato kiasi gani yamepatikana kwenye biashara hiyo?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Serikali inatambua uwepo wa Biashara ya Mtandao. Kwa sasa kuna jumla ya kampuni 1,820 ambazo zimesajiliwa, ambapo kampuni 1,075 za Biashara Mtandao ni shughuli yao kuu na kampuni 745 Biashara Mtandao ni shughuli nyingine. Kwa sasa Serikali inaendelea kuchukua hatua muhimu za kuwa na mfumo madhubuti utakaosimamia biashara hiyo ambayo imeanza kuzaa matunda. Mfano, kwa kipindi cha Julai, 2024 hadi Machi, 2025 Serikali ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 192.78 kutoka kwenye Biashara Mtandao, ambayo inajumuisha betting ya mitandaoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha tunaenda sambamba na kasi ya mabadiliko ya teknolojia kwenye biashara, Serikali imeandaa Mkakati wa Kitaifa wa Biashara Mtandao (National Electronic Commerce Strategy) ambao upo katika hatua za mwisho za ukamilishwaji wake. Maeneo yatakayofanyiwa kazi katika utekelezaji wa mkakati huo ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya TEHAMA, uboreshaji wa Sera, Sheria na Kanuni na pia, uboreshaji wa huduma za mawasiliano, usafirishaji na uchukuzi; uimarishaji wa huduma za miamala kwa njia ya mtandao na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu biashara mtandao, ili waweze kutumia mitandao iliyopo kufanya biashara. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved