Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 173 | 2025-04-29 |
Name
Issa Jumanne Mtemvu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibamba
Primary Question
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Mitaa ya Mpiji Magohe na Saranga katika Jimbo la Kibamba?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Saranga na Kata ya Mbezi, ambayo Mtaa wa Mpiji Magohe upo, hakuna maeneo yaliyotengwa, kwa ajili ya kujenga Vituo vya Polisi. Napenda kutumia fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge, kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, kutenga maeneo ili Serikali iweze kujenga Vituo vya Polisi vya Kata ya Saranga na Kata ya Mbezi, ambayo Mtaa wa Mpiji Magohe upo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved