Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 174 | 2025-04-29 |
Name
Maulid Saleh Ali
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Welezo
Primary Question
MHE. MAULID SALEHE ALI aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi Shehia ya Mtofani katika Jimbo la Welezo Zanzibar?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka utaratibu wa kujenga Vituo vya Polisi daraja C Katika kila Kata na Shehia hapa nchini. Katika Shehia ya Mtofani Jimbo la Welezo Zanzibar hakuna eneo lililotengwa kwa ajili ya kujenga kituo cha Polisi. Ninaomba nitoe wito kwa Halmashauri ya Manispaa ya Magharibi A kutenga eneo, ili Serikali iweze kujenga kituo cha Polisi katika Shehia ya Mtofani. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved