Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 176 | 2025-04-29 |
Name
Innocent Sebba Bilakwate
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyerwa
Primary Question
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-
Je, lini Awamu ya Pili ya Mradi wa Maji wa Rutunguru, Kaisho - Isingiro utaanza ili kuondoa adha wanayoipata wananchi?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mradi wa Maji Kaisho-Isingiro ambayo inahusisha ujenzi wa tanki lenye ujazo wa maji lita 225,000 pamoja na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 17. Lengo la mradi huo ni kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 37,500 waishio kwenye vijiji 11 vya Kaisho, Nyabishenge, Ibare, Ishaka, Karukwanzi A, Karukwanzi B, Kihanga, Kaitambuzi, Katera, Rutunguru pamoja na Nyakakoni. Utekelezaji wa awamu hiyo umefikia 95% na unatarajia kukamilika mwezi Juni, 2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea kutatafuta fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi huo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved