Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 177 | 2025-04-29 |
Name
Godwin Emmanuel Kunambi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlimba
Primary Question
MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:-
Je, lini Serikali itafuta Hati ya Shamba la Balali na kuwakabidhi wananchi wa Melela?
Name
Deogratius John Ndejembi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chamwino
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgogoro wa Shamba la Balali kwa muda mrefu ulikuwa ukishughulikiwa na Serikali ili kuweza kuutatua kiutawala. Hata hivyo, wananchi waliokuwa wanalalamikia shamba hili waliamua kutumia njia ya Mahakama kwa kufungua shauri Mahakama Kuu. Baada ya Mahakama kusikiliza hoja za wananchi hao pamoja na mmiliki wa shamba iliamua kuwa shamba tajwa ni mali ya familia ya Balali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu ulishughulikiwa na Mahakama Kuu Mkoa wa Morogoro kupitia Shauri la Ardhi Na.5 la mwaka 2023. Natoa rai kwa wananchi kuheshimu uamuzi uliotolewa na Mhimili wa Mahakama.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved