Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 178 | 2025-04-29 |
Name
Hawa Subira Mwaifunga
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete Tabora?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Kitete unatekelezwa kwa awamu ambapo hadi sasa Serikali imetoa fedha shilingi bilioni 3.27 ambapo awamu ya kwanza zilitolewa shilingi bilioni 2.69 na awamu ya pili shilingi milioni 578.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha 2024/2025, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete ambapo hadi sasa ujenzi umefikia 50%. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo Februari, 2026.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved