Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 548 | 2025-06-10 |
Name
Naghenjwa Livingstone Kaboyoka
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara za vijijini zilizopo milimani - Same kwa mawe au zege ili kupunguza gharama za kufanya matengenezo?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (NHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Same ni miongoni mwa wilaya ambazo zina mtandao wa barabara zilizoko sehemu za milimani kwenye Tarafa za Mamba, Vunta, Gonja, Chome Suji, Ndungu na Mwembe Mbaga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa Serikali imekwisha jenga barabara za zege zenye urefu wa mita 5,692 kwa gharama ya shilingi bilioni 3.87 katika Barabara za Hedaru – Vunta – Myamba, Mpirani Dispensary – Dindimo Primary School, Maore – Vuje, Maore – Kalungoywo, Msanga – Chome, Hedaru – Makasa, Saweni – Gavao, Ndungu – Lugulu, Kisiwani – Msindo na Suji – Mweteni katika maeneo yenye kona hatarishi za mlima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2025/2026 Serikali imeweka katika mipango yake ujenzi wa barabara za zege zenye urefu wa mita 530 katika Barabara za Bombo – Mpirani, Kizangaze – Mtii, Hedaru – Vunta, Idaru – Narema, Mbuyuni – Marindi na Manka – Madiveni kwa gharama ya shilingi milioni 360.39.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuhudumia barabara na madaraja Wilayani Same kwa kujenga, kukarabati na matengenezo zikiwemo barabara zenye tabaka la zege kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved