Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 180 | 2025-04-29 |
Name
Florent Laurent Kyombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkenge
Primary Question
MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa Uwanja wa Ndege Omukajunguti utaanza?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutatua changamoto za usalama wa Ndege na abiria katika Mkoa wa Kagera, Serikali imeanza utekelezaji wa mpango wa kudumu unaohusisha mjenzi wa kiwanja kipya kitakachokuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa ambapo mnamo mwezi Januari, 2025, Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi iliteua timu ya wataalam kwa lengo la kufanya tathmini ya uchaguzi wa eneo la ujenzi wa kiwanja kipya kikubwa cha Ndege ya Daraja 4C ambacho kitakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa za abiria zinazoweza kubeba hadi abiria 220 kwa wakati mmoja. Pamoja na majukumu mengine, lengo la Kamati hiyo lilikuwa ni kufanya tathmini na kushauri eneo linalofaa kwa ujenzi wa kiwanja hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tathmini ya eneo pendekezwa ambalo ni eneo la Kihabajwa lililopo eneo la Wilaya ya Misenyi imeridhiwa na Serikali na kwa sasa inaendelea na taratibu za utoaji ardhi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja kipya, tayari imeanza kushauriana na Serikali ya Mkoa, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Baada ya zoezi la utoaji ardhi kukamilika taratibu za ujenzi zitaanza mara moja. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved