Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 14 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 181 | 2025-04-29 |
Name
Mashimba Mashauri Ndaki
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Magharibi
Primary Question
MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:-
Je, Serikali inachukua hatua gani na madhubuti kuhakikisha kunakuwa na ushindani kwa wafanyabiashara katika ununuzi wa pamba?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ununuzi wa pamba nchini hufanyika kwa utaratibu wa soko huru ambapo zaidi ya kampuni 35 zimesajiliwa na kupewa leseni ya kununua pamba na usajili unaendelea ili kuongeza ushindani. Kampuni hizi hununua pamba kulingana na hali ya soko ya msimu husika na bei dira iliyokubaliwa na wadau. Aidha, Serikali husimamia na kuhakikisha bei dira iliyokubalika na wadau inazingatiwa katika ununuzi wa pamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na utaratibu huo, Bodi ya Pamba imeingia mikataba na Kampuni za ununuzi wa pamba ambao wameajiri Maafisa Ugani wanaotoa huduma za ugani katika kata zinazozalisha pamba kwa lengo la kuongeza tija na uzalishaji wa zao hilo. Kampuni hizo zinapewa leseni ya kununua pamba katika kata zilizoajiri Maafisa Ugani kulingana na bei dira inayokubaliwa na wadau kwa msimu husika kulingana na bei ya soko. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved