Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 552 | 2025-06-10 |
Name
Deodatus Philip Mwanyika
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Njombe Mjini
Primary Question
MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -
Je, Serikali haioni haja ya kuanzisha eneo mahsusi la viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya misitu?
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inakubaliana na dhana ya kuanzisha eneo mahsusi la viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya misitu kwa kuwa inaendana na mipango ya kuanzisha kongani ya viwanda ikiwa ni pamoja na mpango wa kuendeleza bidhaa za mbao zilizohandisiwa (Engineering Wood Product Framework, 2021-2031), lengo ni kuongeza thamani ya mazao ya misitu kwa kuzalisha bidhaa za mbao handisiwa kama vile veneer, plywood, marine board, blockboard na samani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali imeandaa Mpango Maalum wa Kuendeleza Viwanda unaotarajiwa kutekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026. Kupitia mpango huo imepanga kuanzisha kongani za viwanda ngazi ya halmashauri nchini kulingana na rasilimali zinazopatikana katika halmashauri husika ikiwa ni pamoja na kongani ya viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya misitu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved