Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 553 | 2025-06-10 |
Name
Taska Restituta Mbogo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Je, lini Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa Wilayani Mpanda kwa kutoa maji Bwawa la Milala?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Serikali imeanza utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Manispaa ya Mpanda, Mkoani Katavi. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) katika Bwawa la Milala lenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 13 kwa siku, ujenzi wa miundombinu ya kutibu maji (water treatment plant) yenye uwezo wa kutibu maji lita milioni 12 kwa siku, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 115 sanjari na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 2,000,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 40% na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2025 na kunufaisha zaidi ya wananchi wapatao 245,764 waishio katika Manispaa ya Mpanda. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved