Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 554 | 2025-06-10 |
Name
Josephat Sinkamba Kandege
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalambo
Primary Question
MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa skimu za umwagiliaji utaanza na kukamilika katika maeneo yote ya Wilaya ya Kalambo yaliyobainishwa kuwa na fursa za kilimo?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, katika mwaka 2024/2025 Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini ikiwemo upembuzi yakinifu na usanifu wa Skimu za Ilimba, Mkowe, Santamaria, Sopa, Kamawe, Kasanga, Katete, Mtuntumbe, Kasitu, Tatanda, Mao, Katazi, Mnazi, Kaluko, Kilesha, Kambo, Kalembe, Ulumi na Katuka zenye ukubwa wa jumla ya hekta 21,300 zilizopo katika Wilaya ya Kalambo. Upembuzi wa skimu hizo unatarajiwa kukamilika mwaka 2025/2026 na kuanza taratibu za kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi. Aidha, mradi wa Skimu ya Selengoma yenye ukubwa wa hekta 1,500 iliyopo katika Wilaya ya Kalambo upo katika hatua ya ununuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ujenzi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved