Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 556 | 2025-06-10 |
Name
Antipas Zeno Mngungusi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Malinyi
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -
Je, kwa nini Serikali isijenge mitaro katika Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Namtumbo ili kuinusuru isiendelee kuharibiwa na mvua?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo - Lumecha (kilometa 284.5), sehemu ya Ifakara – Lupiro – Mtimbira (kilometa 112) kwa utaratibu wa sanifu na jenga (design and build). Ujenzi wa barabara hii utaenda pamoja na ujenzi wa mitaro kulingana na usanifu ulivyoelekeza. Kwa sehemu iliyobaki ya barabara hii, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) itaendelea kuijenga mitaro kwa sehemu zenye uhitaji ili kuilinda barabara isiharibiwe na maji ya mvua, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved