Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 43 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 557 2025-06-10

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: -

Je, Serikali imeweka utaratibu gani wa kuwatambua wakandarasi wazawa wanaofanya kazi nzuri ili kuwapa motisha?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) huwatambua makandarasi wanaofanya kazi nzuri kwa kuwapatia tuzo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tuzo za ukuaji haraka kwa wale wanaoonesha ukuaji mzuri tangu usajili, tuzo kwa wakandarasi wanaozingatia usalama kazini na tuzo kwa ajili ya kumpuni zinazomilikiwa na wanawake zenye mafanikio katika miradi. Aidha, mkandarasi anapokamilisha kazi aliyopewa vizuri kulingana na mkataba mwajiri hutoa hati maalum ya kukamilisha kazi (Final Completion Certificate) ambayo hutambua kuwa kakamilisha kazi yake vizuri.