Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 19 | Sitting 43 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 557 | 2025-06-10 |
Name
Stephen Lujwahuka Byabato
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: -
Je, Serikali imeweka utaratibu gani wa kuwatambua wakandarasi wazawa wanaofanya kazi nzuri ili kuwapa motisha?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI Alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) huwatambua makandarasi wanaofanya kazi nzuri kwa kuwapatia tuzo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tuzo za ukuaji haraka kwa wale wanaoonesha ukuaji mzuri tangu usajili, tuzo kwa wakandarasi wanaozingatia usalama kazini na tuzo kwa ajili ya kumpuni zinazomilikiwa na wanawake zenye mafanikio katika miradi. Aidha, mkandarasi anapokamilisha kazi aliyopewa vizuri kulingana na mkataba mwajiri hutoa hati maalum ya kukamilisha kazi (Final Completion Certificate) ambayo hutambua kuwa kakamilisha kazi yake vizuri.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved