Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Stephen Lujwahuka Byabato
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukoba Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: - Je, Serikali imeweka utaratibu gani wa kuwatambua wakandarasi wazawa wanaofanya kazi nzuri ili kuwapa motisha?
Supplementary Question 1
MHE. STEPHEN L. BYABATO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini ninalo swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bukoba Mjini tulipata pesa takribani shilingi bilioni 12.5 kwa ajili ya ujenzi wa njia nne kutoka katikati ya mji kwenda pembeni. Sasa napenda kufahamu, ni nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha inamuwezesha mkandarasi mzuri anayefanya kazi hiyo mzawa anayeitwa Abemulo Contractors kukamilisha kazi hiyo vizuri na kwa wakati ili na yeye tuweze kumpa pongezi, ahsante sana.
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge Serikali itahakikisha kwamba kazi hiyo inakamilika ya kujenga njia nne na tuna kazi mbili pale, tuna miradi miwili, lakini mkandarasi ni huyo huyo. Kuna Mradi wa …. na huo mradi ambao unatekelezwa kwa fedha ya Serikali 100%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichokifanya sasa hivi, tumeshapeleka hati za madai kwa wenzetu wa Hazina ili aweze kuongeza kasi maana amerudi nyuma, aweze kuongeza kasi na kukamilisha kazi kwa sababu sasa hivi tupo kwenye 40%. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Bukoba, Serikali tutahakikisha kwamba hiyo hazi inakamilika, ahsante. (Makofi)
Name
Abeid Ighondo Ramadhani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Kaskazini
Primary Question
MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: - Je, Serikali imeweka utaratibu gani wa kuwatambua wakandarasi wazawa wanaofanya kazi nzuri ili kuwapa motisha?
Supplementary Question 2
MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naomba kujua ni lini sasa ujenzi wa Barabara ya Igauli – Ilongero kilometa kumi na moja na nusu zitaanza ujenzi wake?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, hii barabara iko kwenye majadiliano, tulishaitangaza, wakandarasi wameshapatikana, tuko kwenye majadiliano ya gharama za kuanza ujenzi kipande hicho cha Singida – Ilongero kilometa 11.5, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved