Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 182 2025-04-30

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara za lami katika Mji Mdogo wa Karatu?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara za lami katika Mji wa Karatu ambapo hadi sasa jumla ya kilometa 3.595 zimejengwa kwa kiwango cha lami ambapo mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali ilijenga barabara yenye urefu wa kilometa 0.610 kwa gharama ya shilingi milioni 500. Aidha, mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali ilijenga barabara yenye urefu wa kilometa 0.725 kwa gharama ya shilingi milioni 475.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Serikali vilevile, inaendelea kujenga barabara yenye urefu wa kilometa 0.710 kwa gharama ya shilingi milioni 469.5. Pia, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imeweka katika mipango yake kujenga barabara yenye urefu wa kilometa 0.9 kwa gharama ya shilingi milioni 604.2.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutekeleza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami katika Mji wa Karatu na miji mingine nchini kulingana na upatikanaji wa fedha.